August 14, 2020


RAUL Jimenez mshambuliaji wa Wolves ameambiwa  kuwa lazima aondoke ndani ya timu hiyo msimu huu kwenye dirisha la usajili ili akapate changamoto mpya sehemu nyingine.

Nyota huyo amekuwa akihusishwa kuibukia ndani ya Klabu ya Liverpool na Manchester United ambazo zimeonyesha kuwa zinahitaji saini yake jambo lililomfanya mchambuzi wa masuala ya michezo kituo cha ESPN raia wa Mexico, Sergio Dipp kumwambia kwamba ni muda wake wa kupata changamoto mpya.

Jimenez amekuwa bora ndani ya Wolves akitupia jumla ya mabao 17 ndani ya Ligi Kuu England na mabao 10 ndani ya  Europa League huku akitoa jumla ya pasi 10 za mabao kwenye mashindano yote.

 Raia huyo wa Mexico mwenye miaka 29 ana nafasi ya kufanya makubwa msimu ujao kutokana na uwezo wake licha ya timu yake kutolewa na Sevilla baada ya kufungwa bao 1-0 kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

“Ni muda wake sasa kuondoka ndani ya Wolves na kwenda kupata changamoto mpya kwenye timu kubwa, uwezo anao ikiwa ataondoka kwa sasa itampa mabadiliko makubwa yeye mwenyewe mbeleni,”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic