August 25, 2020

 


TAYARI mambo yanazidi kupamba moto kwenye masuala ya usajili kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa 2020/21 ambao unatarajiwa kuanza Septemba 6 mwaka huu.

Mpaka sasa kwa timu ambazo zimejipanga kufanya usajili ninaona kwamba zimeweza kufanya kile ambacho zinahitaji jambo ambalo katika hilo sina mashaka nalo .

Jambo la msingi ambalo linapaswa kuzingatiwa katika usajili ambao unafanywa ni kufuata ripoti ya mwalimu, yeye ndiye ambaye anajua kwamba anahitaji aina gani ya wachezaji kwenye kikosi chake.

Wapo wale ambao watafanya usajili kwa kufuata mahitaji yao hilo lipo wazi kwa kuwa ni mambo ambayo yapo kwenye soka letu la Bongo.  Zama hizo muda wake umekwisha halipaswi lipewe nafasi kwa sasa.

Muda wa kufanya kazi kwa utaalamu na kufuata taaluma ya kazi ya mpira ni sasa. Soka letu linazidi kukua kwa kasi ikiwa masuala ya kufanya maamuzi kwa kuwa wewe ni kiongozi haileti picha nzuri kwa afya ya soka letu.

Timu zote ambazo zitafanya usajili kwa mapendekezo yao binafsi wakati wa kujua masuala hayo yanakuja,  mchezo wa mpira hauhitaji mambo mengi zaidi ya vitendo na data ambazo zinaongea ukweli muda wote.

Ndani ya dakika 90 ni muda sahihi uwanjani ambao utatosha kuaminisha mashabiki na wanachama wa timu kwamba huyo aliyeletwa ndani kucheza ni pendekezo la kocha ama kiongozi.

Sababu moja kubwa itakayofanya atambulike kwamba alisajiliwa kwa presha ama chaguo la kiongozi ni muda wake atakaoutumia ndani ya uwanja na kile ambacho atakionyesha pia pale atakapopata muda.

Ipo wazi kwamba kuna wale wachezaji ambao walipata nafasi ya kusajiliwa kwa msimu wa 2019/20 ndani ya timu mbalimbali hawakuwa na nafasi kwenye timu zao mpaka msimu unaisha.

Rekodi zinaonyesha kwamba wapo wachezaji ambao walisajiliwa na timu zao kwa msimu wa 2019/20 na hawajacheza mchezo hata mmoja ndani ya ligi zaidi ya kuishia benchi.

Hii ni mbaya na inatoa picha kwamba hakukuwa na chaguo la mchezaji huyo ndani ya kikosi, pia inaua uwezo wa mchezaji na kurudisha nyuma maendeleo ya soka hasa ikiwa alichukuliwa kutoka kwa timu ambayo ilikuwa inahitaji huduma yake labda kutokana na uchumi kuyumba wakashindwa kubaki na mchezaji.

Kwa viongozi wa timu pia ni somo kwamba mpira wa sasa unahitaji fedha na uwekezaji mkubwa hivyo wanajukumu la kuongeza vyanzo vyao vya mapato ili kuweza kubaki na wachezaji ambao wanawahitaji pale msimu unapokwisha.

Tukiachana na timu na mchezaji pia ana kazi ya kuangalia nafasi yake kule anakokwenda asifikirie kupata mkwanja huku nafasi yake ya kucheza akiiweka kapuni itampoteza kwenye ramani ya mpira.

Kwa kuwa maisha ya soka lazima yaendelee mchezaji mmoja kutoka na kwenda kwenye timu nyingine ni muda sahihi wa kila mchezaji ambaye anakwenda kuanza maisha mapya.

Imani yangu ni kwamba mpaka pale dirisha la usajili litakapofungwa Agosti 31 kila kitu kitakuwa kimekwenda sawa ndani ya timu zote kuanzia zile za Ligi Daraja la Kwanza, Daraja la Pili,Ligi ya Wanawake pamoja na zile zinazoshiriki Ligi Kuu Bara.

Kila mtu atavuna kile atakachokipanda ndani ya uwanja ni wakati wa kuanza maandalizi kwa timu zote kwani muda wa ligi kuanza upo njiani na muda wa dirisha la usajili kufungwa upo karibu.

Ujumbe wangu kwa timu ambazo zimepanda daraja kwa msimu wa 2019/20 zikiwa na uhakika wa kushiriki Ligi Kuu Bara msimu wa 2020/21 zinapaswa zijipange kwelikweli kuleta ushindani.

Gwambina FC na Dodoma Jiji hizi zilipanda jumlajumla kutoka Ligi Daraja la Kwanza huku Ihefu wao wakiweka rekodi ya kushinda mchezo wa playoffs mbele ya Mbao FC wote wanapaswa pongezi lakini wasijisahau.

Kama ambavyo wamepishana na Singida United,Lipuli FC,Ndanda FC,Alliance na Mbao wajifunze kwamba msimu ujao isije ikawa ni zamu yao kuwapisha wengine.

Yote kwa yote wasisahau kwamba makosa makubwa ya timu kupata ushindi ni kwenye maandalizi na usajili hivyo wanapaswa kuwa bora katika usajili wakati huu ambao unaelekea ukingoni pamoja na kuanza maandalizi mapema kujenga timu zao.

Nimeona Gwambina FC wao washamaliza kufanya usajili ambapo wana mchanganyiko wa wachezaji ikiwa ni pamoja na wale ambao walikuwa ndani ya timu pamoja na wazoefu kutoka kwenye ligi kuu hiyo ni sawa kwa kuwa lazima mabadiliko yawepo.

Lakini licha ya kumaliza kufanya usajili mzuri ni muhimu kuwa na mpango kazi makini utakaofanya timu iwe inapata matokeo uwanjani na kuleta ushindani kama ilivyokuwa ndani ya Ligi Daraja la Kwanza.

Tunataka kuona kila timu inafanya maajabu na kupata matokeo mazuri kwenye mechi zote ambazo watacheza iwe nyumbani ama ugenini muhimu kupambana kupata matokeo.

Muda wa kufikiria kwamba bado mpo Ligi Daraja la Kwanza umekwisha kwa sasa ni mapambano ndani ya Ligi Kuu Bara ni muhimu kuweka dira mapema kabla mambo hayajaanza kubadilika.

Mashabiki wenu mtambue kwamba wanajua yapo matokeo matatu, kufungwa, sare na kushinda. Furaha yao kubwa ipo kwenye kushinda basi pambaneni kuwapa mashabiki kile ambacho wanahitaji.

Tunahitaji kuona kwamba msimu wa 2020/21 mnakuja kuleta kitu kipya ambacho ni ushindani bila kujali kwamba mmetoka kumaliza maisha yenu ndani ya Ligi Daraja la Kwanza bado mna nafasi ya kufanya vizuri.

Maandalizi makini yanahitajika kwa ajili ya msimu mpya, usajili pia usipuuzwe

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic