August 16, 2020

 

PAUL Nonga, nyota mpya wa Gwambina FC inayonolewa na Fulgence Novatus, ilimlazimu arudishe nauli kwa mabosi wa Namungo ambao walikuwa wanahitaji saini yake.

 

Nyota huyo aliyekuwa Lipuli, alikuwa anahitajika kwenda kusaini Namungo kabla ya Gwambina FC kumvutia kasi na kumpa mkataba.

Akizungumza na Spoti Xtra, Nonga alisema kuwa awali alikuwa kwenye mazungumzo na Namungo iliyokuwa na nia ya kupata huduma yake, lakini alibadili maamuzi baada ya Gwambina kumfuata rasmi.

 

“Nilikuwa kwenye hatua za mwisho kujiunga na Namungo ila Gwambina walipoonyesha nia niliwaelewa na nikaenda kusaini, kwa kuwa nilitumiwa nauli na Namungo ilinibidi niwarudishie mkwanja wao,” alisema Nonga

1 COMMENTS:

  1. Akili matope namungo wanashiriki mashindano ya Caf huenda angeonekana.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic