August 16, 2020

 



CRIS Mugalu mshambuliaji aliyekuwa anakipiga ndani ya Power Dynamo ya Zambia, leo Agosti 16 ametambulishwa ndani ya Simba.

Nyota huyo amesaini dili la miaka miwili na anaungana na washambuliaji wawili tegemeo ndani ya Simba ambao ni John Bocco na Meddie Kagere.

Bocco na Kagere wamekuwa na pacha nzuri msimu wa 219/20 ambapo wote wapo Kwenye kikosi bora cha msimu.

Kwa pamoja wamehusika Kwenye mabao 31 kati ya 78 yaliyofungwa na Simba ambayo imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Kagere alifunga mabao 22 na Bocco alifunga mabao 9 hivyo nguvu ya ushambuliaji inaongezeka kwa Mabingwa hao wa Ligi mara tatu mfululizo.

7 COMMENTS:

  1. Huyo ni sawa na YIKPE Aliechamka kidogo, kiufupi mmekula za uso hapo hamna mshambuliaji

    ReplyDelete
  2. Mfungaji bora Zambia wakati huyo Yipke wako bomu hakuwai kuwa mfungaji bora sehemu yoyote ile duniani tangu azaliwe na hatokuwa mpk atakufa

    ReplyDelete
  3. Huu usajili simba mtaua jamani kha, au mnataka kwenda kushiriki ligi ya Spain? Tangu lini sisimizi akauliwa kwa shoka?

    ReplyDelete
  4. Karibu kwa mabingwa Mugalo

    ReplyDelete
  5. Mchezaji anaitwa Chrispin MUGALU sio MUGALO. Timu aliyotoka ni LUSAKA DYNAMOS na sio POWER DYNAMO. Msichanganye mambo nyie waandishi.

    ReplyDelete
  6. Tshishimbi vipi jamani? Maana wachezaji wa kimataifa ndio washaisha hivyo!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic