September 4, 2020

 


BREAKING: BABA wa nyota wa Klabu ya Barcelona, Lionel Messi amesema kuwa ishu ya La Liga kutaka mwanae kulipa Euro Milioni 700 ili aweze kuondoka haina uhai kwa kuwa muda wake ulishakwisha.

Babaye Messi, Jorge ambaye ni wakala wa mchezaji huyo amesema kuwa taarifa kuhusu mteja wake kwamba anapaswa kulipa Euro milioni 700 ili aondoke hazina ukweli.

Wakala huyo amesema mwanaye anaweza kuondoka ndani ya kikosi cha Barcelona akiwa mchezaji huru kwenda klabu anayotaka.

Inaelezwa kuwa nyota huyo anahitaji kuondoka ndani ya Barcelona ili kupata changamoto mpya na timu inayotajwa kupata saini yake ni Manchester City.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic