September 4, 2020


 Lionel Messi ametangaza kusalia katika kikosi cha Barcelona kwa msimu wa 2020/2021 kufuatia ugumu wa masuala ya kisheria katika mkataba wake yanayoweka zuio la yeye kuikacha klabu hiyo kwa muda huu.


Nyota huyo alikuwa anataka kuondoka ndani ya Barcelona baada ya timu hiyo kufungwa mabao 8-2 na Klabu ya Bayern Munich kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. 


Katika maelezo yake, Messi amesema “Sikuwa na furaha nikataka kuondoka,nabakia kwenye klabu ili nisiingie kwenye mvutano wa kisheria. Utawala wa Bartomeu ni janga kwa klabu.”


Timu iliyokuwa inapewa nafasi kupata saini ya nyota huyo ilikuwa ni Manchester City.

1 COMMENTS:

  1. Huyo mesi kwel mjanja,amejirud ili amalize mkataba wake wa mwaka moja ili aondoke bure

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic