DESEMBA 16 dirisha la usajili lilifunguliwa rasmi ikiwa ni ruksa kwa timu za Bongo kufanya usajili wa ajili ya wachezaji.Hii ni fursa kwa benchi la ufundi kutoa ripoti na kuchagua aina ya wachezaji ambao wanawahitaji.
Muda pekee wa kufanya maboresho
pale ambapo kuna makosa ni sasa. Hakutakuwa na wakati mwingine kwa timu kuweza
kufanya usajili kwa ajili ya msimu wa 2020/21.
Benchi la ufundi kwa mechi ambazo
zimechezwa limeona wapi pana tatizo. Nina amini kwamba kila kitu kimeweza
kuonekana kwa wakati huu ambapo ligi inaendelea.
Kuanzia kwa timu zinazoshiriki Ligi
Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza, Ligi Daraja la Pili na Ligi Kuu ya Wanawake
Tanzania Bara zote usajili huu unawahusu kwa wakati huu.
Ni wazi kwamba kwa mujibu wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), timu zinazoruhusiwa kufanya usajili kwa sasa
ni zile ambazo hazijakamilisha idadi ya wachezaji wanaotakiwa.
Neno langu ni kwamba mabenchi ya
ufundi ni muhimu kuangalia mapema mahitaji yao yapo kwenye nini kwa wakati huu
ndani ya timu zao.
Kabla sijaenda mbali ninapenda
kuwaomba Watanzania kuendelea kuziombea dua timu ambazo zinapeperusha bendera
ya Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa.
Simba itakuwa na kazi nchini
Zimbabwe na itacheza na FC Platinum, leo Namungo itakuwa na kazi mbele ya El
Hilal Obeid ya Sudani.
Mashabiki ni jukumu letu kuungana
kuwaombea wawakilishi wetu ili wafanye vizuri na wachezaji pia ni jukumu lenu
kupambana kupata matokeo.
Nikirudi kwenye mada ambayo nipo
nayo leo ninaamini kwamba mabenchi ya ufundi yana jukumu kubwa la kuwasilisha
majina ya wachezaji inaowahitaji, kisha uongozi kufanyia kazi katika
kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.
Kwa wachezaji ambao watapata bahati
ya kupata changamoto mpya wana jukumu la kuendeleza juhudi kwenye maisha yao
mapya ambayo wanakwenda kuishi.
Imani yangu ni kwamba benchi la
ufundi litasimamia masuala ya usajili na kupata wachezaji ambao wanahitaji kwa
kufuata taratibu ambazo zimewekwa.
Ikiwa itakuwa hivyo kila mmoja
atakuwa na kazi moja ya kutimiza majukumu yake kwa wakati pale ambapo atapewa
kazi ya kufanya.
Imani yangu kwa zile timu ambazo
zilikuwa zinashindwa kupata matokeo kutokana na kuwa na wachezaji ambao hawana
uzoefu muda ni huu.
Pia ikumbukwe kwamba usajili wa
wakati huu ni mdogo haina maana kwamba kikosi kizima kinasajiliwa hapana ni
usajili kwa nafasi ambazo zipo wazi.
Mapendekezo ambayo yatafanyika na
benchi la ufundi yatajibu ndani ya ligi kwa kuwa suala la mpira ni mchezo wa
wazi.
Kikubwa ambacho kinatakiwa kwa
wachezaji watakaopata nafasi kwenye timu mpya ni kuendeleza juhudi kwenye
kusaka matokeo ndani ya uwanja.
Lengo la timu kwenye usajili wa
mchezaji ni kuona kwamba anapata nafasi ya kuwa ndani ya timu na kufanya yale
ambayo yanaleta matokeo chanya ndani ya uwanja.
Ikiwa mchezaji atashindwa kuishi
kwenye msingi ya mpira itakuwa rahisi kwake kuanguka.Jambo la msingi ni kuona
kwamba kila mchezaji habweteki pale anapopata nafasi.
Kujifunza kwa yale ambayo yaliweza
kukuweka sokoni ni muhimu kupambana na kuendelea kuyafanya muda wote. Hii ni
njia bora ambayo itawafanya wachezaji kuzidi kuwa kwenye ubora wao.
Kuwa na kipaji ni muhimu na
kuendeleza kipaji ni muhimu pia kwa kuwa kisipoendelezwa ni rahisi kupotea.
Benchi la ufundi pia ikiwa
litafanya usajili mzuri basi yale malalamiko kwamba wanashindwa kupata matokeo
kwa kuwa hawana wachezaji wenye uzoefu nina amini litakwisha.
Ipo wazi kwamba kuna timu ambazo
mwendo wake ni wa kusuasua ndani ya ligi kwenye kusaka matokeo. Nyingine mwendo
wao ni kupwa na kujaa.
Leo inafanya vizuri kesho inakwama kuendelea pale ilipoishia hivyo inakuwa inakwenda mbele na kurudi nyuma.
Ushindani ndani ya ligi ni mkubwa
hakuna ambaye hajui lakini ni muhimu na timu kuwa na mwendelezo mzuri kwenye
kusaka matokeo ndani ya uwanja.
Kwa wakati huu mfupi ambao
hautadumu kwa muda mrefu ni mrefu pia kwa wale ambao watautumia kwa umakini.
Kwa timu ambazo zina kazi kimataifa
leo nina amini zitapambana kusaka matokeo kwa kuwa matokeo mazuri ni furaha kwa
Tanzania.
0 COMMENTS:
Post a Comment