December 10, 2020


DIRISHA la usajili la Ligi Kuu Bara linatarajiwa kufunguliwa Desemba 15 ambapo kwa sasa unaweza kusema kwamba bado siku sita kuweza kufikia siku ya dirisha hilo kufunguliwa.

Kuna umuhimu mkubwa kwa kila timu kuanza maandalizi mapema kwani matokeo chanya uwanjani yanatengenezwa na maandalizi ya awali ambayo timu huwa zinafanya.

Muda wa kufanya haya yote ni sasa kwa kuanza kujipanga ili kuweza kufanya usajili makini kwa wakati huu wa kufanya maboresho ndani ya timu.

Kwa timu zote bila kujali zinashiriki Ligi Kuu Bara ama Ligi Daraja la kwanza ni muhimu kujipanga vema.

Wale ambao wamekuwa wakifanya usajili kwa matakwa yao ama kutumia nafasi zao za uongozi si sawa kwani anayejua uhitaji wa wachezaji ni kocha mwenyewe.

Itapendeza endapo viongozi watafuata ripoti ya kocha kwenye kufanya usajili jambo liakaloepusha lawama na malalamiko kwa benchi la ufundi kwani wao ndio wanahusika kwenye suala la kupanga timu.

Kwa kupitia yale mapungufu ambayo benchi la ufundi limeyaona hapo ndipo kazi inabidi ifanyike na sio kusajili kwa kufuata mkumbo.

Kila mmoja amekuwa ana mamlaka hasa linapofika suala la usajili kulingana na mapenzi ambayo anayo kwa mchezaji ama wengine ni wale ambao wanaona kwamba watapata faida endapo watamsajili mchezaji fulani.

Sasa suala la kutazama faida huwa linakuwa kwa muda tu tofauti na yule ambaye atasajili kwa kufuata mapendekezo ya mwalimu itasaidia kujenga kikosi imara.

Ikumbukwe kuwa wakati timu ikiboronga anayepewa mzigo wa lawama siku zote huwa ni mwalimu hivyo itakuwa vizuri endapo ripoti itafanya kazi lawama zitakuwa haziepukiki kwake.

Kwa wakati huu timu nyingi zimeona namna ambavyo zilikuwa kwenye kusaka pointi tatu ndani ya uwanja pamoja na matokeo ambayo wamekuwa wakiyapata.

Jambo la kuzingatia kwa sasa ni wachezaji makini na wazuri ambao watakuwa na nidhamu nje na ndani ya uwanja hii itasaidia kuwa na benchi makini pamoja na timu imara.

Muda mzuri kwa Shirikiso la Mpira Tanzania (TFF) kuendelea kutoa taarifa mapema na masuala yote yanayohusu usajili kwa wanachama wake kwa wakati huu.

Ikumbukwe kwamba kuna timu ambazo zimepanda daraja msimu huu ikiwa ni pamoja na Gwambina FC, Ihefu,Dodoma Jiji hizi nazo pia zina jukumu ya kuangalia pale ambapo zimekuwa na mapungufu.

Suala la kukurupuka kwenye usajili kwa wakati huu litakuja kutoa majibu baada ya ligi kumalizika kwa kuwa dirisha dogo siku zote hutumika kufanya maboresho kidogo na sio kikosi kizima.

Kama wachezaji watatukuwa kwenye mazungumzo na timu ni muhimu kuangalia sehemu ambayo wanakwenda pamoja na nafasi yake huko.

Wachezaji wanatambua kwamba wakati unaokuja ni muda wa mauzo hilo lipo wazi lakini lazima wasisahau kwamba kazi yao ni mpira hivyo lazima wacheze.

Wakati wa usajili pia ni muda wa kuonyesha kwamba thamani ya mchezaji uwanjani ilikuaje na nanmna gani anaweza kuwa msaada kule anakokwenda jambo la msingi ni kujitambua.

Ikitokea mchezaji akapata timu na akakubaliana kuwa mchezaji wa hiyo timu anayokwenda basi lazima aendane na utaratibu ambao ataukuta maisha ya mchezaji ambaye hatambui kazi yake ni magumu kwa wakati ujao.

Kila kitu kwenye soka kinawezekana na ipo wazi kwa muda huu malipo ya wachezaji yawe wazi na wajitoe kwa moyo mmoja kufanya kazi na kutafuta matokeo.

Benchi la ufundi litazame namna bora ya kufanya kuweza kusajili wachezaji makini ambao watasajiliwa kupitia ripoti ambazo zimeandaliwa.

Nidhamu inapaswa ipewe kipaumbele na wachezaji wawe makini kuelekea kwenye maisha yao mapya ambayo watakwenda kuanza ni muhimu kuzingatia kwamba maisha yanakwenda kasi sana.

Jambo la msingi kwa viongozi na mabosi wa timu kuzingatia usajili kwa kufuata ripoti na sio mapenzi ya timu ama kiongozi fulani.

Wawakilishi wa kimataifa Simba na Namungo wana jukumu pia la kuweza kufanya maboresho kwenye vikosi vyao ili kuweza kufanya vizuri kwenye hatua za mbele.

Tayari nina amini kwamba benchi la ufundi limeona mapungufu ambayo yapo kwenye timu zao hivyo jukumu lao ni kwenye kuboresha vikosi.

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic