SAIDO Ntibanzokiza ingizo jipya ndani ya Klabu ya Simba akitokea nchini Burundi kwa kusaini dili la miaka miwili amesema kuwa atashirikiana na wachezaji wenzake ili kufanya vizuri zaidi.
Akiwa amecheza mechi mbili za Ligi Kuu Bara baada ya kusaini dili hilo akiwa ni mchezaji huru ila alikuwa anafanya mazoezi na Klabu ya Vital O ya Burundi, amehusika kwenye mabao manne kati ya 28 yaliyofungwa na Yanga.
Amefunga bao moja na kutoa pasi tatu za bao.Mchezo wake wa kwanza ilikuwa ni dhidi ya Dodoma Jiji ambapo alifunga bao moja na kutoa pasi moja ya bao.
Mchezo wake wa pili ilikuwa ni dhidi ya Ihefu FC ambapo alitoa jumla ya pasi mbili za mabao Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Nyota huyo amesema kuwa atashirikiana na wachezaji wenzake kuendelea kufanya vizuri.
"Bado kuna kazi ya kufanya ndani ya Yanga, nina amini kwamba mashabiki wanahitaji kuona timu inapata matokeo nami nitafanya hivyo.
"Kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu nina amini kwamba tutafanya vizuri hivyo mashabiki waendelee kutupa sapoti," .
Mwandishi umekosea ingizo jipya ndani ya Simba au yanga
ReplyDeleteSAIDO Ntibanzokiza ingizo jipya ndani ya Klabu ya Simba
ReplyDeleteHuyu mwandishi hata shule hajaenda anashindwa kutofautisha kati ya Simba na yanga
ReplyDelete