December 2, 2020




UONGOZI  wa yanga upo katika harakati za kuhamishia mechi zao zilizobaki za Ligi Kuu Tanzania Bara jijini Arusha baada ya kudai kubaini hujuma wanayofanyiwa Dar.


Habari za kutoka ndani ya Yanga zinasema wamekuwa wakishinda kwa tabu kunatokana na njama chafu zinazofanywa na wapinzani wao, zinazosababisha wachezaji kuchoka kabla ya dakika 90 kumalizika.


“Tunadhani kuna mtu yupo ndani yetu anatumiwa, tena inawezekana tupo naye kila siku na anajipenyeza hadi kambini Kigamboni." kilisema chanzo chetu.

Alipotafutwa Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrik Mwakalebela ili aweze kuzungumzia juu ya suala hilo la timu ya Yanga kuwa kwenye mpango wa kuhama Dar aliweka wazi kuwa hakuna mpango huo. 


"Kuhusu kuhama Dar na kuelekea Arusha kwa sasa hapana, hakuna mpango huo," .


22 COMMENTS:

  1. Pumzi imekata. Visingizio vimeanza.Hata muhamie Burundi haisaidii.

    ReplyDelete
  2. Ngoja mme wenu amalize na plateu and awachokonoe hko juu acheni kuweweseka

    ReplyDelete
  3. Hakuna timu hapo mfukuzeni senzo huyo

    ReplyDelete
  4. Ni hapo mwizi anapoogopa kuibiwa

    ReplyDelete
  5. Utopolo hali tete, na bado sana. Mtahamia Mtwara.

    ReplyDelete
  6. Wote ni zero! Chanzo cha habari wapi?

    ReplyDelete
  7. Wachezaji pumzi inakata mapema kipindi cha pili fanyieni kazi hili badala ya kutafuta sababu za nje ya mchezo hazisaidii saaana

    ReplyDelete
  8. Tulieni na kila mtavobabaika ndipo mtavozidi kuanguka. Msiwasikilize waganga na nyie ndio mnaoutaka ubingwa. Watakumalizeni

    ReplyDelete
  9. Kwani huko Arusha ndio Kuna nini na hiyo Ruvu Shooting watakubali kuburuzwa huko Arusha? Tulieni na mumtimuwe haraka huyo mbaya wenu nasi tumjue

    ReplyDelete
  10. Mbona hata mikoani mnashinda kwa taabu? Kama anayewahujumu yupo karibu yenu, hata huko Arusha mtakuwa naye.

    ReplyDelete
  11. Mechi za mikoani wanshinda kwa ushindi wa namna ganij

    ReplyDelete
  12. Shari huzaa Shari na chakula chake ni shari

    ReplyDelete
  13. Hongera Yanga. Baada kuifanyia hujuma Simba na wao kubaini na kuziba mianya ya hujuma kwa kuwafukuza mawakala wake.sasa na nyinyi mmebaini kuwa inawezekana Simba inaweza kulipiza. Hongereni mmeshtuka mapema. Simba walichelewa mkawachezea katika michezo karibu mitatu

    ReplyDelete
  14. Hii taarifa Yanga wamekanusha. Hawahami Dar kuigopa hujuma bali watacheza mechi zao mbili mikoani. Kanuni inaruhusu timu kuchagua uwanja wowote kwa mechi mbili ndio maana KMC walipeleka mechi yao na Yanga jijini Mwanza. Pia mwaka juzi African Lyon walipeleka Arusha mechi zao dhidi ya Yanga na Simba. Au kwakuwa Yanga ndio mnaandika na visababu vya uongo mbona hamkuhoji why KMC mechi kapeleka Mwanza?

    ReplyDelete
  15. Hii blog 80% ya habari zake ni za kubumba

    ReplyDelete
  16. Utopolo chali ngoja muanze kugongwa kila mechi, maana hata nje ya dar goli ni hilohilo moja tu. Mtafukuzana muda cmrefu wanaume twaja.

    ReplyDelete
  17. Hakuna lolote saleh anabangaiza habari za kuandika. Angalia huko chini alivoishia hakuna kitu. Yanga haiwezi kuhamishia mechi Arusha. Timu haijapoteza game yoyote kuna haja gani ya kusema hayo? Huyu ni mwandishi mbumbaji tu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic