KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Miraji Athuman ambaye anatajwa kuwekwa kwenye rada za mabosi wa Namungo leo Desemba 27 anatimiza miaka 27 ya kuletwa duniani.
Msimu huu wa 2020/21 mambo yamekuwa magumu kwake kupata namba kikosi cha kwanza tofauti na msimu uliopita ambapo alikuwa na nafasi kikosi cha kwanza.
2019/20 alitupia mabao 7 na kutoa pasi moja ya bao majeraha ya mara kwa mara ni moja ya sababu iliyomtoa kwenye reli. Kwa msimu huu wa 2020/21 hajafanikiwa kutupia ndani ya Ligi Kuu Bara.
Huenda mipango ya Namungo ikijibu ya kumuhitaji nyota huyo kwa mkopo anaweza kuendeleza makali yake kwenye kikosi hicho kinachonolewa na Hemed Morroco.
0 COMMENTS:
Post a Comment