JUMA Mwambusi, kocha msaidizi wa Yanga amesema kuwa wanahitaji kumaliza mechi za mzunguko wa pili bila kupoteza.
Yanga imekamilisha mzunguko kwa kucheza jumla ya mechi 17 ambazo
ni dakika 1,530 bila kupoteza ikishinda mechi 13 na kulazimisha sare nne.
Safari yake ya mzunguko wa pili itaanza Desemba 31 ambapo
itakuwa na kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Tanzania Prisons, Uwanja wa
Nelson Mandela.
Mwambusi amesema kuwa:”Tunatambua kwamba
tumemaliza mzunguko wa kwanza bila kupoteza, hesabu zetu ni kuona kwambe
kwenye mchezo wetu ujao ni lazima tupambane ili kupata matokeo chanya zaidi,” ,
Mchezo wa kwanza walipokutana Uwanja wa Mkapa, Yanga
ililazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Tanzania Prisons.
0 COMMENTS:
Post a Comment