March 24, 2021


 WAKATI kipa wa Simba, Aishi Manula akiendelea kung’ara kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, taarifa kutoka Sudan zinasema kwamba, Rais wa Al Merrikh, Adam Sudacal, ametoa takribani shilingi 230 kuinasa saini yake.

 

Waarabu hao wa Sudan, wanaonekana kuwa siriaz katika kuinasa saini ya Manula baada ya kutengeneza rekodi ya kutoruhusu bao katika mechi tatu za hatua ya makundi ya michuano hiyo msimu huu.

 

Chanzo makini kimeliambia Spoti Xtra kuwa, Kocha Mkuu wa Al Merrikh, Lee Clark, amemuomba rais wa klabu hiyo, Adam Sudacal ampatie nafasi ya kumsajili Manula ili aendelee kukiboresha kikosi chake jambo ambalo amekubaliwa na kinachosubiriwa ni Simba kupokea ofa yake.


“Kuna uwezekano mkubwa wa Manula kutokuwa naye msimu ujao endapo Simba watakubali ofa ya Al Merrikh ambao wanamtaka kipa huyo.


“Dau lao waliloweka ni dola laki moja ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 230, za Kitanzania” kilisema Chanzo hicho.

 

Msimu huu Manula amekuwa kwenye kiwango bora katika michuano hiyo ambapo mpaka sasa amecheza jumla ya mechi saba na kuruhusu bao moja tu dhidi ya FC Platinum hatua ya mtoano. Ana clean sheet sita. Mkataba wake unaisha 2022.


Manula kwa sasa yupo na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ambayo kesho ina mchezo dhidi ya Equatorial Guinea ambao ni kwa ajili ya kufuzu Afcon.

6 COMMENTS:

  1. Yaan utoke timu kubwa ukacheze timu ndogo? atakuwa chizi

    ReplyDelete
  2. Na pesa je mbona hauzungumzii kama anatoka ndogo kwenda kubwa? Au unamaanisha Manula anacheza kwa sifa akizeeka anakuwa hana kitu kama Ngasa?

    ReplyDelete
  3. Auzwe tununue wengine kama metacha anafaa kusaidiana na kakolanya

    ReplyDelete
  4. Al Merrikh sio timu ndogo nyie

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic