MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Wydad Casablanca ya Morocco, Mtanzania, Simon Msuva amefichua kuwa ndoto zake msimu huu ni kuhakikisha anakuwa mfungaji bora kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Msuva mpaka sasa ameshafunga mabao mawili katika hatua ya makundi ya michuano hiyo na timu yake ipo kundi C.
Msuva amesema kuwa malengo yao katika michuano hiyo ni kuchukua ubingwa pamoja na kuwa mfungaji bora kutokana na kuanza vizuri.
“Kwanza Wydad ni timu kubwa ambayo itanifanya nionekane zaidi na tunashiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, malengo yetu ni kuchukua ubingwa wa Afrika lakini pia ubingwa wa Morocco.
“Lakini nashukuru nimeweza kuanza vizuri na tayari nimeshafunga mabao mawili katika hatua ya makundi na sasa matumaini yangu ni kuendelea kupambana ili ikiwezekana niwe mfungaji bora wa michuao hii ambayo itaongeza kitu kwenye wasifu ‘CV’ wangu,” amesema Msuva.
Msuva pambana tu ndugu lakini ujue huku kwetu Tanzania kuna vijana wanakiwasha aiseee,kwahiyo unatakiwa kujipanga MZEE.
ReplyDeleteDa ume mwambia ukwel kna chamana luis ni atal ana mawil 2 wakat wenzie wana 3
DeleteKwa kwel kaka msuva hiyo nafasi ni ngumu Ila matumaini ni bora
ReplyDeletePambana bro hata Mimi naamin hvoo
ReplyDeletePambana wewe ndio bendela yetu,tunakuombea
ReplyDelete