May 2, 2021


 MENEJA wa mshambuliaji wa Yanga, Mghana, Michael Sarpong, Alex Kamanzi raia wa Rwanda ameibuka na kusema kuwa hana presha yoyote juu ya mwenendo wa mchezaji wake katika timu hiyo kwa kuwa hata waajiri wake hamna walichomweleza hadi sasa kuhusu mustakabali wake.

 

Sarpong mpaka sasa katika ligi kuu amefanikiwa kufunga mabao manne pekee licha ya kuwa na rekodi kubwa kabla ya kutua Yanga kutokana na kufunga mabao 23 katika Ligi Kuu ya Rwanda akiwa na Rayon Sport.


 Kamanzi amesema kuwa kwa upande wake hana presha yoyote licha ya mteja wake kushindwa kuwa na kiwango kizuri cha kufunga mabao katika timu hiyo kwa kuwa bado hawajaelezwa chochote hadi sasa.

 

“Unajua hakuna ambacho tumeelezwa na Yanga hadi sasa hivyo tunaendelea kusubiri kwa sababu ndiyo jambo jema kwetu haijalishi kuna presha kiasi gani kutoka katika upande wa mashabiki ndiyo maana tunasubiri kuona itakuwaje baadaye.

 

“Kikubwa tunamuomba juu ya kuwepo kwa presha ili aweze kupata nafasi na pia imekuwa nzuri kwa kuwa hayupo kwenye majeruhi yoyote, naamini anapitia kipindi cha mpito ambacho atakaa sawa tofauti na inavyochukuliwa na wangine,” amesema Kamanzi.


Kwa sasa Yanga ipo kwenye maandalizi ya mchezo wa ligi dhidi ya Simba amabo unatarajiwa kuchezwa Mei 8, Uwanja wa Mkapa.

3 COMMENTS:

  1. Na atacheza mechi ya Simba utake usitake

    ReplyDelete
  2. Mr Wakala - mteja wako amelogwa, muulize mwenendo wa maisha yake binafsi inawezekana kuna mahali aliharibu na akaishia kurogwa.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic