June 18, 2021




ANAANDIKA kipa namba moja wa Yanga, Metacha Mnata kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram:- Kwa niaba ya Familia yangu, Management yangu na mimi mwenyewe napenda kuchukua fursa hii kuomba msamaha kwa Viongozi wa Klabu yangu ya Yanga SC, Wachezaji wenzangu, Benchi la Ufundi, Mashabiki wa Klabu ya Yanga, Mamlaka za soka nchini na wadau wote soka ambao wamekwazika kwa kwa kitendo nilichokifanya jana.


Nikiri hakikuwa kitendo cha kiungwana hivyo najutia makosa niliyoyafanya. Mimi kama mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa napaswa kuwa mfano mzuri siku zote mbele za watoto na wanaotamani kuwa kama mimi na watu ambao aidha walikuwepo kiwanjani au waliona mechi kupitia Televisheni majumbani kwao.

Natambua mchango na umuhimu wa mashabiki kwangu binafsi na kwa Klabu, hivyo kitendo kile hakikupaswa kutokea.

Natanguliza Shukrani 🙏
#DaimaMbeleNyumaMwiko

Mnata kutokana na kitendo hicho ambapo alikaa langoni na ubao ukasoma Ruvu Shooting 2-3 Yanga alionekana akiwatendea kitendo kisicho cha kiungwana mashabiki wakati wa kutoka Uwanja wa Mkapa.
Kutokana na kitendo hicho uongozi wa Yanga, jana Juni 17 ulitoa taarifa ya kumsimamisha nyota huyo kwa muda usiojulikana.

11 COMMENTS:

  1. Nenda tuu, si unarubuniwa na wale wa timu ya taifa

    ReplyDelete
  2. Nakumbuka kitendo kama hicho ni mwaka jana tu kiliwahi kufanywa na mchezaji na TFF ikampa adhabu ya kufungiwa michezo kadha je adhabu kama hiyo inatumika bado?

    ReplyDelete
  3. Tusubiri tuone kama adhabu kwa kila ataetenda kosa kama hilo

    ReplyDelete
  4. Huu ndio uungwana...Naomba nikukumbushe mapito aliyopitia mwenzako Aishi Manula kipindi fulani ambapo yalimkuta kama yaliyokukuta wewe ambapo mashabiki wa Simba walisahau mema yote aliyoyafanya hadi kufikia hatua ya kumzomea na kutaka asipangwe kwenye mechi lakini alivumilia matusi ya mashabiki na wala hakujibizana nao isipokuwa aliyafanyia kazi mapungufu yake na matokeo yake akageuka kuwa shujaa na kipenzi chao wakati wa michuano ya ligi ya mabingwa Africa na hata mechi za ndani za ligi.
    Asilimia 80 ya mashabiki wa soka(hasa wa Tanzania) ni mbumbumbu wasiojua a be che de za mpira kwa hiyo inahitaji busara nyingi kukabiliana nao,wamesahau zile penalt ulizookoa na makosa ya wazi ya mabeki zako uliyoyafuta na kuikoa timu katika mechi mbali mbali.
    Umeanguka inuka uangalie kilichokufanya ujikwae kisha fanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza na usonge mbele.DAIMA KUMBUKA MASHABIKI WA SOKA KOTE DUNIANI MCHANGO WAO MKUBWA KWA WACHEZAJI NI LAWAMA NA ASILIMIA NDOGO NI PONGEZI NA SHUKRANI.

    ReplyDelete
    Replies
    1. We c useme tu mashaabiki wa utopolo, usiogope

      Delete
    2. Mikia kushinda nyuma aka paka mweusi

      Delete
  5. Hahaha usiwaogope makahaba wa Gsm wewe dole la kati lile halifutiki

    ReplyDelete
  6. Sijafahamu alichosema "mikia kudhinda nyuma, aka paka mweusi" nini maana yake?

    ReplyDelete
  7. Yes..Sasa umekua na hio ndio busara.Good boy

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic