July 30, 2021

 KIUNGO Christian Eriksen anatarajiwa kurejea kwenye timu yake ya Inter Milan kwa ajili ya kufanyiwa vipimo ili aweze kurudi uwanjani kuendelea na majukumu yake.



Ericksen alidondoka kwenye mchezo wa Euro 2020 akiwa anaitumikia Denmark na baadaye ilielezwa kuwa anasumbuliwa na matatizo ya moyo.

Inter Milan wamesema kwamba pamoja na kwamba mchezaji huyo amekuwa akipata matibabu lakini wenyewe wanatakiwa kumfanyia vipimo upya kabla ya kurejea uwanjani.


Timu hiyo imesema kuwa inataka kutambua ni tatizo gani ambalo lilimpata nyota huyo wakiamini kuwa anaweza kurejea uwanjani kwa nguvu.


Kwa sasa nyota huyo mwenye miaka 29 yupo jijini Copenhagen baada ya kuondoka hospital mwezi uliopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic