July 6, 2021

 


KOCHA mkuu wa kikosi cha Simba, Didier Gomes amefunguka kuwa ni kweli walitarajia kukutana na mchezo mgumu dhidi ya Yanga, lakini hakutarajia kwamba wangeweza kuwapa presha kubwa mwanzoni mwa mchezo, hali ambayo iliwatoa mchezoni wachezaji wake.

Simba juzi Jumamosi ilipoteza nafasi ya kutangaza ubingwa wake wa nne mfulululizo baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya watani zao wa jadi Yanga, kwenye mchezo wa kiporo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye uwanja wa Mkapa Dar es Salaam.

Licha ya matokeo hayo ya kipigo, Simba imeendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara na pointi zao 73 walizokusanya katika michezo 30 waliyocheza mpaka sasa, na wanahitaji pointi tatu kutangaza ubingwa hivyo watalazimika kujiuliza tena dhidi ya klabu ya KMC keshokutwa Jumatano.

Akizungumzia mchezo huo, Gomes amesema: “Ni kweli nilitarajia kukutana na mchezo wa presha kubwa kutoka kwa Yanga kwenye mchezo wetu wa Jumamosi, lakini niweke wazi kuwa sikutarajia kama wangeweza kuanza mchezo wakiwa na presha kubwa namna ile.

“Hali hii iliwatoa mchezoni wachezaji wangu kiasi kwamba kwa dakika 30 za kwanza ni kama vile hatukuwa uwanjani, na kwa bahati mbaya tulikuwa tayari tumetanguliwa bao moja dhidi yao, hivyo hata tulipokuja kurejea mchezoni japo tulijitahidi lakini tulishindwa kusawazisha kwa kuwa walikuwa na nidhamu kubwa ya ulinzi.

“Mchezo huo umeisha na sasa tunajipanga na mchezo wetu wa Jumatano, ambao ni wazi utakuwa muhimu kwetu kutangaza ubingwa.”

 

3 COMMENTS:

  1. Wambie hao mashabiki zako wenyew wanafikir kufungwa na yanga eti ni uchawi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Uchawi alitangaza mpili, kama ni mshabiki wa simba sawa

      Delete
  2. IMEVUJA: Julai 25 mtu anapigwa 4G

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic