July 31, 2021



WAKATI yakisubiriwa kwa hamu maamuzi ya Mahakama ya kimataifa ya Usuluhishi wa Michezo (CAS), kuhusiana na kesi ya Yanga dhidi ya kiungo mshambuliaji wa Simba, Bernard Morrison kila upande umeonekana kuwa na matumaini makubwa ya kushinda huku tambo zikiendelea kutembea.

Kesi hiyo yenye usajili wa CAS 2020/A/7397 ilisikilizwa juzi Alhamisi Juni 29, mwaka huu ambapo baada ya kusikiliza mashauri ya pande zote mbili, mahakama hiyo iliweka wazi kuwa majibu ya kesi hiyo yatatolewa katika kipindi ya kati ya kesho Agosti mosi, mpaka Agosti 24, mwaka huu.

Katika kesi hiyo Uongozi wa klabu ya soka ya Yanga unadai uliingia na makubaliano ya mkataba wa miaka miwili na mchezaji huyo, huku Morrison yeye akidai kuwa mkataba wake halali ulikuwa wa miezi sita pekee.

Akizungumzia ishu hiyo Ofisa habari wa klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli amesema: “Tunamshukuru Mungu kesi imeenda vizuri na baada ya taratibu zote za mashauri ya kesi kufanyika, sasa hivi utaratibu wa kawaida wa kufanya tathimini ya ushahidi uliotolewa hivyo watatoa maamuzi kati ya Agosti mosi, mpaka 24 mwaka huu.

“Ni kweli hatuwezi kuzungumzia hatima ya kesi hii, lakini tuna matumaini makubwa haki itatendeka hivyo Wanayanga wanapaswa kuwa watulivu wakati huu mahakama ikiwa inafanya maamuzi yake.”

Katika kilichoonekana kuwa ni kijembe kwa Yanga, Morrison naye kupitia mtandao wa Instagrama ameandika: “Hata katika wingi wa maji, bado mjinga ataendelea kuhisi kiu.”

13 COMMENTS:

  1. Achaa anyooshwe, alitaka aombewe.

    ReplyDelete
  2. Replies
    1. wewe ndio akili zako fupi,yanga wanatafuta haki haki yao bwege mkubwa we

      Delete
  3. Wanangojea ubingwa wanyanganywe Simba wapewe wao na Morrison kwa nguvu arejeshwe kwao kweli ni akili hiyo au ndoto ya bangi?

    ReplyDelete
    Replies
    1. huna akili wewe mahakama ziliwekwa za kazi gani acha yanga watafute haki na mtanyooshwa tu

      Delete
  4. Watanyoka utopolo wanashida kweli bumbuli ajipange kufatwa na takukulu

    ReplyDelete
  5. Hahahahhhhhh et hata kwenye wingi wa maji mjinga bado atahisi kiu

    ReplyDelete
    Replies
    1. atahisi kiu yeye mwehu anayevua bukta uwanjani

      Delete
  6. Yang waache kupoteza mda. Mbn wachezaj WAP weng .ten wazur zaid at ya b3

    ReplyDelete
    Replies
    1. sio kupoteza muda vicha kama akina morrison lazima tuwanyooshe

      Delete
  7. Haishi kutapatapa, atulie asubiri hukumu

    ReplyDelete
  8. kama anajifanya mwendawazimu mwaka huu yanga itamtibu na mikia watamuona shubiri

    ReplyDelete
  9. Hata hivyo Morrison alitoa hiyo comment kabla kesi haijasikilizwa....ilikuwa kabla ya kesi

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic