July 5, 2021

 


RASMI mabosi wa Azam FC wamemalizana na kiungo wa Zambia Charlse Zulu kwa dili la miaka miwili.


Kiungo hiyo jana Julai 4 alifanyiwa vipimo na kuweza kufuzu hivyo wakafikia makubaliano ya kumpa kandarasi ya miaka miwili.


Alikuwa anakipiga ndani ya Klabu ya Cape Town City ya Afrika Kusini hivyo msimu ujao wa 2021/22 atakuwa ndani ya viunga vya Azam Complex.


Azam FC wamemalizana naye baada ya kufikia makubaliano na timu yake ya Cape Town City aliyokuwa akitumikia ambapo pia aliwahi kukipiga ndani ya Zanaco ya Zambia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic