July 13, 2021


 NAHODHA wa KMC, Juma Kaseja ambaye alikaa langoni Julai 7 na kuokota mabao mawili yaliyofungwa na Chris Mugalu amesema kuwa wapinzani wao wangetulia Simba wangewafunga mabao mengi kipindi cha kwanza.


Kaseja ambaye ni Tanzania One aliweka wazi kwamba kwenye mchezo huo wa ligi wakati ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma KMC 0-2 Simba, timu yao ilifanya makosa mengi kipindi cha kwanza.


“Kipindi cha kwanza tulifanya makosa mengi sana na kama wapinzani wetu wangekuwa makini kwa nafasi ambazo walizipata basi wangetufunga mabao mengi kwa kutumia makosa yetu.


“Lakini kipindi cha pili ilikuwa ngumu kwao kutufunga kwa kuwa makosa ambayo tulifanya kipindi cha kwanza tulifanyia kazi hivyo walishindwa kutufunga, nasi tulishinwa kuwafunga,” amesema.


Kocha Msaidizi wa KMC, Habib Kondo amesema kuwa walifungwa kwa kuwa walishindwa kutengeneza nafasi jambo ambalo watalifanyia kazi kwenye mechi zao mbili zilizobaki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic