KUFUATIA kukosekana kwa kocha wa makipa wa Simba, Milton Nienov aliyepata matatizo ya kifamilia, mlinda mlango namba moja wa kikosi hicho, Aishi Manula ndiye amebebeshwa mikoba ya ukocha wa makipa, kwa kuongoza mazoezi ya makipa wa timu hiyo wakati wa maandalizi ya mchezo wao wa leo jioni dhidi ya Yanga.
Kocha Nienov alikosekana kwenye mchezo wa jana dhidi ya Yanga kufuatia kuondoka kwa ruhusa maalum, ya kushughulikia masuala ya kifamilia kwao nchini Brazili.
Katika mazoezi ya Simba ambayo tuliyashuhuhudia Manula alionekana kuchukua jukumu la
kuongoza programu za mazoezi hayo kwa kuwaongoza wenzake, Beno Kakolanya na
Ally Salim.
0 COMMENTS:
Post a Comment