September 29, 2021


BREAKING:MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ndani ya Klabu ya Simba, Mohamed Dewji ameamua kukaa pembeni kwenye nafasi hiyo kutokana na makubaliano ya Bodi ya Wakurugenzi ndani ya Simba.


Taarifa ambayo ameituma Mo amesema kuwa:"Miaka minne tumepata mafanikio makubwa,tumeshinda ligi mara nne kufanya vizuri Champion League,(Ligi ya Mabingwa Afrika).

"Bado ninaipenda Simba. Tumefanya mkutano wa bodi tarehe 21,9,2021 tumekubaliana kwamba mimi nitastep down, (kuwa pembeni) kuwa chairman (mwenyekiti) Simba SC.

"Ninaomba wanachama wa Simba msifikirie mimi ninaondoka kwenye Simba, mimi bado ni mwanahisa, ninaipenda Simba, tumekubaliana kufanya hivyo kwa sababu mimi nimekuwa ninasafiri sana," .


9 COMMENTS:

  1. Replies
    1. Mo anahela ila Salum be Try again yupo vizuri Zaidi kiungozi kwa hivyo hakuja haribika kitu.

      Delete
    2. Atuambie kwanza akina Chama na Miquissone wameuzwa shilingi ngapi na Fedha za mauzo zipo Akaunti ipi?

      Delete
  2. MAJUKUMU NI MENGI, MALI ZA FAMILIA, HUKU TIMU, UNADHANI KAZI NYEPESI?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwani miaka yote minne alikuwa hayo majukumu nani alikuwa anayafanya?

      Delete
  3. Mo Dewji ni tajiri wa kweli. Kama unamuuza Chama na Kondeboy ukarudisha pesa yako kidogo kwa nini uendelee kupata hasara tena? Unalipa kocha, wachezaji na kila kitu bado marefa, uchawi na mambo kibao faida utapata lini? Ameonyesha uwezo wake wa kufikiri na kwa nini yeye ni tajiri." Tafakari na chukua hatua"

    ReplyDelete
  4. Amesoma alama za nyakati. Maana mayai viza na maneno ya shombo vinafuatia sasa maana ufalme wa simba umefika kikomo

    ReplyDelete
  5. ha ha ha ha ha, kachomoa betri huyo hana lolote miaka yote minne alikuwa hasafiri???

    ReplyDelete
  6. Mmmmh kusafiriiii??????👀👀👀

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic