October 10, 2021


LEO Oktoba 10 kikosi cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi kinatarajiwa kujipima ubavu na timu ya JKU  SC katika mchezo wa kirafiki unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Azam Complex.

Wachezaji ambao wamebaki kambini Dar katika kijiji cha Avic Town ikiwa ni pamoja na Mayele, Abdul Shaibu, 'Ninja', Paul Godfrey, 'Boxer' watakuwa na kazi ya kujiweka sawa na kuonyesha uwezo wao.

Mchezo huo wa kirafiki unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 1:00 usiku na utakuwa live Azam TV.

Kwa upande wa kiingilio kwenye mchezo huo mzunguko ni buku tatu pekee, (3,000) na VIP 5,000,(buku tano).

Mastaa ambao wapo kwenye majukumu yao ya taifa ikiwa ni pamoja na Dickson Job, Bakari Mwamnyeto, Feisal Salum hawa hawatakuwepo kwenye kikosi cha leo.

1 COMMENTS:

  1. Mchezo utachezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, sio Uwanja wa Chamazi. Rekebisheni hiyo.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic