April 20, 2025

 


SIMBA SC v Stellenbosch FC ni mchezo wa nusu fainali ya wababe wawili 2024/25 kimataifa wakiwa na rekodi yakumfungashia virago bingwa mtetezi kwenye mashindano ya kimataifa kwa nyakati tofauti.

Aprili 20 2025 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa uwanja wa New Amaan Complex huku Simba SC ya Tanzania ikiwa na rekodi yakumfangashia virago Zamalek 2003 kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na Stellenbosch FC wamemfungashia virago Zamalek kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.

NENO LA SEMAJI AHMED ALLY

Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo huo na wasiwe na presha kwa timu hiyo kutoka Dar na kwenda visiwani.

“Niwaombe watu wa Zanzibar na hasa mashabiki wa Simba SC wafanye kila kinachowezekana kuipeleka Simba fainali. Nilisema kila kizazi na historia yake, hii imekuja wakati muafaka na sisi kuandika historia ya kuipeleka Simba SC  fainali. Tufanye kila kinachowezekana Mnyama kwenda fainali.

“Mpinzani wetu Stellenbosch FC sio timu dhaifu, hadi inafika hatua hii inaonyesha ni timu ambayo imejiandaa. Wanasimba wote tulijiandaa kucheza na Zamalek lakini Stellenbosch FC akammaliza pale pale nyumbani kwake. Hajamtoa Zamalek kwa bahati mbaya.

“Ni kweli ni timu ngeni lakini ina wachezaji wenye ubora mkubwa na wana kocha mkubwa. Tuna kazi kubwa kwelikweli kuhakikisha tunamthibiti, tunamfunga ili tukienda kwenye mechi ya ugenini ni iyenaiyena hadi fainali.

WALIFIKAJE HAPO

Simba SC ilipita hatua ya nusu fainali kwa ushindi wa jumla ya penati 4-1 dhidi ya Al Masry baada ya mchezo wa kwanza ugenini ubao kusoma Al Masry 2-0 Simba, robo fainali ya pili ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 2-0 Al Masry hivyo mshindi alipatikana kwa penati.

Stellenbosch FC wao walipata ushindi kwenye mchezo dhidi ya Zamalek ambao walikuwa ni mabingwa watetezi walitolewa kwa kufungwa bao 1-0 wakiwa nyumbani Aprili 9 2025 baada ya ile robo fainali ya kwanza ubao kusoma 0-0 kwa timu zote mbili Aprili 2.

 

KAULI MBIU YA SIMBA SC

Kaulimbiu ya kuingia nusu ilikuwa HII TUNAVUKA na Simba SC ikafanikiwa, kuelekea fainali Simba SC kaulimbiu yao inasema HATUISHII HAPA.

Ahmed ameongeza kuwa malengo makubwa ni kuona kwamba wanatoka katika hatua ya nusu fainali na kufika hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

SIRI YA SIMBA KUTINGA NUSU FAINALI

“Kila mtu ni siri yake anajua alifanya nini Simba kufika nusu fainali. Wachezaji wanajua walipambana vipi Simba SC inafika nusu fainali, viongozi wanajua walipambana vipi, benchi la ufundi linajua lilitumia mikakati gani. Rai yangu kila alichofanya mtu kuipeleka nusu fainali kwenye mechi hii ya kuipeleka fainali basi azidishe mara tatu yake.

“Inawezekana sana Simba SC kucheza fainali sababu ubora huo tunao na kila kitu kimekaa vizuri. Na bahati nzuri fainali tutaanzia ugenini na kumalizia nyumbani. Tushindwe nini? Haleluya

Nafasi ya nne Afrika bado sio malengo ya Simba, nusu fainali bado sio malengo ni sehemu ya mapito. Tunaitaka nafasi ya kwanza Afrika, sio rahisi kumfikia wa kwanza sababu ya alama alizonazo lakini tunaanza na kusogea nafasi ya tatu au ya pili lakini kufikia hilo tunaanza na mchezo wa nusu fainali.

SABABU YA KUHAMA UWANJA

“Kuhama uwanja wapo watu wameanza kuingiwa ubaridi sababu ya kuhama uwanja, msemo wa Kwa Mkapa Hatoki Mtu umewaingia Wanasimba, kuhamia Uwanja wa Amaan Simba SC itakuwa na ubora wake uleule. Nipo hapa kuwatoa hofu Wanasimba kwamba kanzu ndio imebadilika lakini sheikh ni yule yule.

“Mnyama ni yule yule na malengo yetu ni yale yale kumfanya vibaya Stellenbosch FC. Asitokee Mwanasimba kuwa na wasiwasi. Ambacho tungemfanya Stellenbosch katika Uwanja wa Mkapa ndio tutamfanya Uwanja wa Amaan. Wao waje uwanjani kushangilia mengine watuachie sisi.

 

 “Ambacho tungemfanya Stellenbosch katika Uwanja wa Mkapa ndio tutamfanya Uwanja wa Amaan. Wao waje uwanjani kushangilia mengine watuachie sisi.

“Kama mnavyojua kulitokea changamoto katika mchezo uliopita hivyo Simba SC tukachagua Uwanja wa Amaan sababu ni bora lakini pia ni nyumbani pia kwa Simba. Kikosi cha Simba kitawasili Zanzibar kesho asubuhi, tumeamua kuja mapema ili kujiandaa na wachezaji waanze kuzoea mazingira ya Zanzibar.

“Stellenbosch FC bado hawajatupa taarifa kama watakuja moja kwa moja Zanzibar au watapitia Dar es Salaam. Simba SC tunacheza nusu fainali ya michuano ya CAF baada ya miaka mingi kupita, mwaka 1993. Tunayo furaha kubwa sana ya kuingia nusu fainali, hii ni hatua kubwa sana sababu inakuza ukubwa wa Simba na wote mmeona tumepanda ubora kutoka nafasi ya saba hadi nafasi ya nne."

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic