June 28, 2016





MPIRA UMEKWISHAAAAA
-SUB, Mazembe wanamuingiza Badibake
-KADI Assale analambwa kadi ya njanoDAKIKA 4+ ZA NYONGEZA
KADI Dk 89 Ulimwengu analambwa kadi ya njano
Dk 85 na 86, TP Mazembe wanaonekana kuupoza mchezo taratibu kama wameridhika na bao moja. Lakini Yanga wawe makini na mashambulizi ya kushitukiza

Dk 84, Ulimwengu anawatoka  Twite na Bossou na kupuga kupiga shuti, Yanga washukuru unatoka juu kidogo. Ilikuwa hatari sana
Dk 82, Kamusoko anapiga faulo safi kabisa hapa...goal kick
Dk 80, Niyonzima anaangushwa nje ya eneo la hatari, mwamuzi anasema faulo. Si mbali sana na lango la Mazembe
SUB Dk 78 Mazembe wanamtoa Adama Traore na nafasi yake inachukuliwa na Deo Kanda
Dk 76, Ulimwengu anaingia vizuri hapa anapiga shuti linakuwa butu
GOOOOOOOOOO Dk 73, Bope anaukwamisha mpira wavuni baada ya kujichanganya kuokoa baada ya mpira wa faulo
KADI Dk 72 Yondani analambwa kadi ya njano

Dk 72, Yondani anamuweka Ulimwengu chini hapa, inakuwa ni ni, faulo nje kudogo ya eneo la hatari
SUB Dk 71 Yanga wanamtoa Chirwa anaingia Simon Matheo
Dk 70, Assale tena, anaingia vizuri na kupiga shuti kali kabisa hapa
SUB Dk 69 Yanga wanamtoa Mahadhi aliyeumia na nafasi yake inachukuliwa na Mwashiuya
Dk 69, Ulimwengu anajaribu hapa shuti, goal kick
Dk 68, Ulimwengu anamtoka hapa Yondani lakini Kamusoko anawahi na kuokoa

KADI Dk 66, Twite anakuwa mchezaji wa kwanza kulambwa kadi ya njano
Dk 60 na 61, mashambulizi ya zamu kwa kila mlango, lakini hakuna shambulizi kali kwa kuwa mabeki wanaokoa kwa urahisi kabisa
Dk 59, kona inachongwa, Yanga wanachelewa kuokoa lakini Nekandio anashindwa kulenga lango na kuwa goal kick
Dk 58, pasi nzuri ya Mahadhi lakini Asale anatoa na kuwa kona, inachongwa, Koulibaly anaokoa

Dk 55, Kasusula anamuangusha Mahadhi hapa, mwamuzi anasema faulo, anaichonga faulo Niyonzima, lakini laini kabisa
Dk 53, Asalle akiwa nje ya 18 ya Yanga anaachia shuti kali lakini anashindwa kulenga lango
Dk 51 hadi 52, Yanga wanamiliki mpira kwa dakika mbili zote, hata hivyo mipango ya umaliziaji inaonekana bado
Dk 50, MAzembe wanapata kona, inachongwa na Asale, hatari hapa lakini Twite anaokoa
Dk 47, Mazembe wanaonekana kuanza kufanya mashambulizi na Yanga wanapaswa kuwa makini na mipira ya juu
Dk 45 Kipindi cha pili Yanga wanaonekana kuanza kwa kasi kabisa hapa. Ngoma anakwenda chini baada ya kuumizwa

MAPUMZIKO
-Nafasi nyingine bora kabisa, Yanga wanapoteza, Kaseke na Ngoma wanashindwa kuwa na mawasiliano ndani ya 18 ya Mazembe hapa

DAKIKA 1+ YA NYONGEZA
Dk 45, Asale anachonga kona nyanya kabisa hapa, inakuwa goal kick
Dk 44 KAsusula anaichonga vizuri, Dida anawahi kuanguka lakini anaugusa na kuwa kona, inachongwa Twite anaokoa, kona tena
Dk 43, Asale alikuwa anakwenda hapa lakini Mahadhi anamwangu na kuwa faulo
Dk 42 Ulimwengu anaingia vizuri akiwa amebanwa na Yondani lakini anafanikiwa kupiga shuti, si kali sana

Dk 39 hadi 41, bado hakuna ubunifu sana kwa kipa upande na muda huu wote mpira umechezwa katikati
Dk 37 na 38, TP wanaonekana kuupoza mpira huku wakijipanga kwa pasi za taratibu. Lakini mabeki wanafanya kosa hapa na kipa anatoka na kuokoa
Dk 36, Twite anapiga shuti kali la mpira wa adhabu...goal kick

KADI 35 Mpeko analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Chirwa
Dk Dk 34, krosi nzuri ya Juma Abdul, Ngoma anaukosa mpira akiwa hatua tatu kutoka langoni. Hii ni nafasi nzuri zaidi ambayo Yanga wamepoteza
Dk 30, Kaseke anaingia vizuri, kona. Inachongwa vizuri na Niyonzima lakini Mazembe wanaokoa hapa
Dk 28, Kamusoko anafanya kazi ya ziada kuondoa mpira miguuni mwa Traore, agauke na mpira na kuondosha
KADI Dk 27, Adama Traore wa MAzembe analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Juma Abdul

Dk 23 hadi 24, Yanga ndiyo wanaonekana kuucheza sana mpira, lakini bado hawana mipango ya umaliziaji
Dk 22 Chirwa anawatoka mabeki wa TP, kwake Ngoma, anapiga krosi safi, Mahadhi hatari hapa. Mpira anauwahi Niyonzima unarudi na kukumuta Juma Abdul, anapiga shuti linaokolewa, anapiga tena TP wanaokoa hapa

Dk 20, Traore anaingia tena kwenye lango anaingia na kupiga krosi safi, Dida anaokoa na Bossou anatoa na kuwa kona...
Dk 15, Niyonzima anaingiza krosi safi kabisa lakini kipa anatoka na kuokoa. ...faulo
Dk 12, Yondani anashika, mwamuzi anasema faulo kwenda Yanga, anapiga Kasusula, hovyoooo kabisa
Dk 11, hatari hapa, Chirwa anaingia lakini Mazembe wanaokoa, Mahadhi anaingia tena, kona. Inachongwa lakini haina matunda

Dk 9, Juma Mahadhi anaingia vizuri kabisa lakini MAzembe wanatoa na kuwa kona. Inachongwa, Bossou hatariiiii lakini inakuwa goal kick
Dk 7, Kipa Guela anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa faulo wa Kamusoko na kuwa kona. Inachongwa vizuri hapa, goal kick..
Dk 5, Traore anaingia kwa kumtoka Juma abdul, anapiga krosi safi kabisa, kona. Inachongwa na Asale, off side
Dk 4, Mazembe wanagongeana vizuri na kuingia kwenye hatari la Yanga, mpira unatoka na kuwa goal kick lakini wachezaji wa TP wanalalamika kuwa ni kona

Dk 3, Yanga wanakuwa wa kwanza kujaribu, Juma Abdul anapiga shuti kali la mpira wa adhabu....juuu
Dk 2, hakuna timu iliyofanikiwa kugusa kwenye lango la mwenzake hadi dakika 2 na nusu za mchezo



Mechi ndiyo imeanza na kila upande unaonekana kuanza kwa umakini kabisa



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic