August 2, 2016



Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye ameweka wazi anachoamini ni bora katika mabadiliko yaliyofanywa na wanachama wa kalabu ya Simba.

Wanachama wa klabu ya Simba wamepitisha kwa pamoja kuwa klabu yao kuingia kwenye mfumo wa kampuni na hisa kuanza kuuzwa hasa ikiwa ni siku chaache baada ya mfanyabiashara maarufu, Mohammed Dewji ‘Mo’ kutangaza hadharani nia yake ya kutaka kununua hisa asilimia 51 kwa Sh bilioni 20.

Nape ameandika kupitia mtandao wa Twitter akieleza uamuzi huo wa wanachama wa Simba kama utasimamiwa kwa uhakika utakuwa na tija.

Huku akisisitiza mfumo mpya kama utasimiwa utakuwa na tija kwa mashabiki wa Simba kununua hisa, ikiwa ni maana maendeleo ya Simba yanaweza kuchagishwa na Wanasimba wenyewe.

Kauli hiyo ya Nape, inaonyesha wazi inaunga mkono uamuzi wa wanachama hao wa Simba walioupitisha katika mkutano wa mwaka wa wanachama Jumapili iliyopita.


Lakini anaweka msisitizo katika usimamizi bora kwenye katika mfumo huo ili kuufanya kuwa na tisa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic