March 17, 2013




Kiungo wa AEK Athens, Giorgos Katidis amefungiwa kutokana na kushangilia kwa kutumia saluti ya kinazi.

Katidis alionyesha ishara hiyo ya jeshi la zamani la Nazi lililokuwa chini ya Fashist Adolf Hitler na leo Shirikisho la Soka la Ugiriki limetangaza kumfungia maisha kuichezea timu zote za timu ya taifa.

Kiungo huyo mwenye miaka 20 tayari amesema hakuwa na nia mbaya huku akilaani vyombo vya habari kulikuza suala hilo.

Yeye amesisitiza alikuwa akimuonyesha kidole mchezaji mwenzake, Michalis Pavlis aliyekuwa mbele yake kwa lengo la kuonyesha furaha yake.

Klabu yake tayari imeeleza inasubiri maelezo kutoka kwa kiungo huyo ambaye siku hiyo alifunga bao la ushindi kwa timu yake hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic