March 17, 2013


 *Kutoka India atupa madongo kwa waliomuondoa madarakani…

PAMOJA na mashabiki 698 kumuondoa madarakani Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage na kuikabidhi timu kwa Mwenyekiti, Zacharia Hans Pope na Makamu wake, Rahma Al Kharusi ‘Malkia wa Nyuki’, yeye ameibuka na kupiga.

Rage ambaye yuko katika matibabu nchini India ameibuka na kusema waliofanya hivyo hawajafanya taratibu huku akiporomosha maneno ya dharau kwamba, wamefanya mkutano wao uchochoroni huku akiulinganisha sawa na ule wa harusi.

“Ni mtu mmoja tu anayeweza kuitisha mkutano, ni Ismail Aden Rage na wala si mtu mwingine. Kwa hiyo Wanasimba watulie nikirudi nitajua cha kufanya,” alisema ambaye yuko kwenye matibabu nchini India.


“Wangekuwa wanajua wana haki basi wangefanyia mkutano, wameenda vichochoroni, ndiyo maana nasema mkutano huo ni wa uchochoroni, hakuna kitu kama hicho,” alisema Rage ambaye anarajia kutua nchini wiki ijayo

Leo mchana wanachama hao, wengi waliokutana ni kutoka katika tawi la Mpira Pesa ambaow amekuwa na upinzani mkubwa na Rage.

Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Star Light Cinema jijini Dar es Salaam, waliamua Hans  Pope na Malkia washike nafasi hizo.

Hata hivyo,  tayari Hans Pope amesema hataweza kuchukua nafasi hiyo na kuwataka wavute subira lakini pia imeelezwa hata Malkia we Nyuki ametaka kuwe na subira.
Tayari aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ ametangaza kujiuzulu, wiki moja na ushee iliyopita.

Lakini Rage ameonekana ni mgumu kama ‘nyundo’ kujiuzulu huku idadi kubwa ya wanachama wakiwa wanashauri apumzike.

wanachama hao walifikia uamuzi wa pamoja kuuondoa madarakani uongozi huo, kutokana na kile kilichoelezwa kushindwa kutekeleza majukumu yao na kuifikisha timu pabaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic