March 13, 2013

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho, Azam FC wamewasili salama salimini nchini Liberia tayari kwa mechi yao dhidi ya Barrack YC II.

Mmiliki wa wa timu hiyo ni kati ya watu wenye uwezo kifedha nchini humo, ingawa hata hivyo inaonekana Barrack YC ni kati ya timu change zinazochipukia kwa kasi.

Msemaji wa Azam FC, Jaffari Idd Maganga amesema kikosi hicho kimetua salama nchini humo na wanajiandaa na mechi hiyo Jumamosi mjini Monrovia.

Azam imefanikiwa kuvuka hatua moja baada ya kuitoa kwa aibu Al Nasiri ya Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 8-1.

Watoto hao wa Bakhresa walianza na ushindi wa mabao 3-1 nyumbani jijini Dar es Salaam, kabla ya kutoa kipigo kikali cha mabao 5-0 walipokuwa ugenini mjini Juba.

Azam FC inaonekana kuwa na maandalizi ya kutosha, ingawa inaonekana italazimika kufanya kazi ya ziada kuwashinda Waliberia hao kwa kuwa ni timu wasiyoijua na si maarufu sana kuweza kupata taarifa zake za kutosha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic