March 13, 2013




Kiatu alichokuwa amevaa beki mkongwe wa Yanga, Stephano Mwasyika, hivi karibuni kilizua gumzo kubwa kwa mashabiki waliokuwa wamehudhuria mazoezi hayo kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Mashabiki walianzisha mjadala wakihoji kama kiatu hicho kilikuwa kikimtosha Mwasyika, ilionekana ni kama oversize.

“Mwasyika anakimbiaje, kile kiatu ni kama kikubwa sana, hebu angalia jamaa anavyokimbia,” alisema shabiki mmoja na wengine wakaangua kicheko.

Muda mwingi, waliendelea kumfuatilia Mwasyika, ambaye hata hivyo alionekana kucheza vizuri ingawa kwa kumuangalia, kiatu hicho kilionekana ni kikubwa kweli.
Wakati mashabiki hao wanaendelea na mjadala wao huku wakimfuatilia hatua kwa hatua, Mwasyika alipata pasi nzuri kutoka kwa Said Bahanuzi, naye aliachia shuti kali lililomshinda Said Mohammed na kujaa wavuni.

Lilikuwa shuti kali lililowashitua wengi waliokuwa uwanjani hapo na kulazimika kumshangilia.
Shabiki mwingine akasema: “Kumbe kiatu chenyewe kiko fiti (akimaanisha kinamtosha), kama kingekuwa kinapwaya asingepiga shuti kali kama hilo.”

Baadaye iligundulikwa kiatu hicho cha Mwasyika ni aina ya Puma asili yake nchini Ujerumani na si Lotto kama ambavyo baadhi ya mashabiki walieleza awali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic