March 14, 2013




Timu ya Azam FC iko tayari kwa vita kabla ya kuivaa Barrack Young Controllers siku ya Jumapili mjini Monrovia.

Lakini uongozi wa timu hiyo umelazimika kubadili hoteli ukiachana na ile iliyoandaliwa na wenyeji wake.

Kwa mujibu wa uongozi wa Azam FC, hoteli hiyo ilikuwa si nzuri ingawa wangeweza kukaa, lakini kulichowakwaza ni harufu kali ya rangi.

Wameeleza inaonyesha rangi katika hoteli hiyo ilikuwa imepakwa siku chache zilizopita, hali iliyofanya kuwe na harufu kali ya rangi na mafuta ya taa.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Azam FC ulitaka kubadilishiwa hoteli, lakini Barrack Young Controllers wakasema wameshalipa kila kitu, hivyo wasingeweza kufanya mabadiliko yoyote.

Kutokana na hali hiyo, Azam FC ikachukua uamuzi wa kusonga mbele zaidi na kutafuta hoteli nyingine.

Azam imefika hatua hiyo baada ya kuing'oa Al Nasiri ya Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 8-1 katika mechi zilizochezwa Dar es Salaam na Juba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic