March 13, 2013



Wababe wa Uturuki wanaongozwa na Didier Drogba, wamefanikiwa kusonga mbele hadi hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Galatasaray iliyolazimishwa sare ya mabao 1-1 nyumbani, wamesonga mbele baada ya kushinda ugenini dhidi ya Schalke 04 ya Ujerumani kwa mabao 3-2.

Mabao ya Galatasaray yalifungwa na Altintop katika dakika 37, Yilmaz (dakika 42), Bulut (dakika 90).

Mchezaji mwingine maarufu Mwafrika anayechezea Emmanuel Ebou aliyewahi kung’ara akiwa na Arsenal ya England.


Pamoja na Eboue, mwingine alinyeng’ara katika kikosi hicho jana ni kiungo Wesley Sneider, Mholanzi ambaye aligoma kutua Man United na kujiunga na Waturuki hao.

Baada ya sare ya mabao 1-1, wadau wengi waliipa nafasi Schalke 04 ya kusonga hadi robo fainali. Wajerumani hao walifanya vizuri zaidi katika hatua ya makundi.

 KIKOSI CHA GALATASARAY:
Galatasaray: Muslera, Eboue, Kaya (Zan 78), Nounkeu, Riera, Felipe Melo, Altintop, Sneijder (Amrabat 70), Inan, Drogba na Burak Yilmaz (Bulut 86).
Subs haikutumika: Iscan, Balta, Kurtulus, Sarioglu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic