March 13, 2013




Kama utabishi basi ni tabia yako, lakini huyu jamaa anaitwa Lionel Messi ni zaidi ya hatari, alichoifanya AC Milan, hatari sana!

Barcelona imeonyesha ni timu yenye uwezo mkubwa licha ya kupoteza mechi zake mbili dhidi ya Real Madrid, pia ya tatu dhidi ya AC Milan, hali iliyosababisha wengi kuamini imeporomoka kiwango.


Lakini jana, Barcelona imeitandika AC Milan kwa mabao 4-0 na kufanya iibuke na ushindi we mabao 4-2, baada ya kuwa imepoteza mechi yake ya kwanza mjini Milan kwa mabao 2-0.
Baada ya kupoteza mchezo huo, wengi waliamini Barcelona ilikuwa imetoka katika hatua hiyo ya Ligi ya Mabingwa hatua ya 16 Bora na isingeweza kusonga hadi robo fainali.


Messi ndiye alikuwa kiwembe baada ya kufunga bao katika dakika ya 5 tu ya mchezo akionyesha ufundi wa hali ya juu, lakini akipa msumari wa pili katika dakika ya 40.

Waitaliano hao walienda mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao hayo mawili, kipindi cha pili kiliponza, dakika ya 55, David Villa akapachika bao la tatu na kuivusha Barcelona.
Lakini ilionekana mapambano yanaendelea na huenda AC Milan angeweza kutibua mambo.

Huku AC Milan wakiwa wamepanda mbele na kutaka kusawazisha kwa hali na mali, wakapigwa kaunta atak, beki we kushoto Jordi Alba akamaliza kazi na kufunga bao la nne.

Maana yake, matumaini ya AC Milan yakawa yametoweka na uthibitisho Barcelona imesonga mbele kama ilivyo kwa wapinzani wao wakubwa Real Madrid.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic