March 12, 2013




Siku chache baada ya mambo kuanza kwenda mlama na viongozi kadhaa kuanza kujiuzulu, hali ya hofu na kuhujumiwa imeanza kutanda ndani ya Simba.

Inaonekana mambo si mazuri kwa maana kuna watu ambao ni mashabiki au wadau wa klabu hiyo wameanza hujuma za chinichini ili kuipoteza Simba njia.

Mmoja wa viongozi wa Simba, hakutaka kutajwa ameeleza kuwa wako katika uchunguzi ili kubaini nyendo za wanaowahujumu kutokana na hofu waliyoanza kuipata.


“Kweli tuna hofu, huenda mambo si mazuri na kuna viongozi walio madarakani au waliojiuzulu hawataki maendeleo ya klabu. Inawezekana wako wanaotaka kuonyesha kuondoka kwao kutasababisha Simba isiwe na amani.

“Simba ina watu wengi sana, inaweza kwenda bila ya mtu mmoja. Sasa hatuwezi kusema ni nani, lakini lazima tufanye uchunguzi kuangalia inakuwaje.
“Kuna taarifa tumeletewa, kwamba kuna mmoja wa viongozi wa zamani wa Simba ameanza kuhujumu na ana urafiki na wachezaji wetu. Sasa hili ni tatizo, lakini siku ya mwisho tutabaini, ndiyo maana hatuwezi kutaja majina,” alisema kiongozi huyo.

Lakini mdau mwingine wa Simba, amesema moja ya hofu kubwa kwamba kuna hujuma, ni wachezaji wakongwe kuwa na sababu nyingi siku chache kabla ya mechi ya Coastal Union.

“Wachezaji wakongwe walianza taratibu kujiondoa kwenye timu na kutoa sababu ambazo siku ya mwisho zilisababisha timu iwe na vijana tu. Lakini tukacheza na kushinda.

“Lakini utaona pia, timu kabla haijaenda uwanjani tukazuiliwa pale hotelini, Dhaira, Mudde na Basena nao wakatimuliwa hotelini. Kama mwepesi kung’amua, jiulize kwa nini mambo haya yanayotekea sasa.

“Kweli hili jambo linashangaza, lakini ni picha inayoonyesha kiasi gani viongozi wetu wanavyokuwa watu wanaojifikiria wao tu bila ya kujali wengine. Hawataki Simba ifanye vizuri, kisa wao hawapo. Ni kitu kibaya sana na kinazidi kuwafunua wasivyo waaminifu.

“Sisi tunajua, katika wale ambao hawako Simba leo, kiongozi mmoja wa zamani ameanza kuwa tatizo. Tutafanya kila tunachoweza kumkamata, hatuwezi kukubali kudhalilishwa au kuharibiwa mambo kwa kuwa tu eti yeye hayupo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic