March 13, 2013




Kijana mwingine wa Tunisia, amejimwagia mafuta na kujipiga kiberiti mbele ya hadhira, hali ambayo imewakumbusha wengi tukio la kijana, Mohamed Bouazizi aliyejiunguza na kusababisha machafuko Tunisia ambayo yalisababisha kuondolewa kwa Rais Abidine Ben Ali wa nchi hiyo na baadaye yakatambaa Afrika ya Kaskazini karibu yote, hasa nchi za Kiarabu.

Kijana huyo anayekadiriwa kuwa na miaka 27, hakujulikana jina lake lakini ni maarufu sana kwa mchezo wa soka, na imeelezwa kwa England amekuwa shabiki namba moja wa Manchester United.

Pamoja na kuipenda Manchester United, kijana huyo ni shabiki wa Marseille we Ufaransa na anajulikana sana kutokana na mapenzi yake ya soka.

Kilichosababisha kijana huyo kuchukua uamuzi mgumu kama huo ni kukosa kazi baada ya kufanya hivyo kwa kipindi kirefu bila ya mafanikio.


Alikuwa akisumbuka kutafuta kazi katika eneo la mji wa Jandouba alikokulia, lakini alitoka na kusafiri katika miji kadhaa bila ya mafanikio.

Mwisho alichukua uamuzi wa kujichoma moto mbele ya watu, juhudi za kumzima zilifanyika na baadaye akakimbizwa katika hospitali kwa ajili ya matibabu.

Aliungua sana, haraka hata kwa kumwangalia inaonekana anahitaji matibabu makini na ya hali ya juu ili kuokoa maisha yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic