March 13, 2013




Viongozi wa Simba wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kukanusha mambo mengi, lakini hali halisi iko hivi, mshambuliaji wake, Felix Mumba Sunzu ameondoka nchini kimyakimya.

Sunzu ameondoka bila ya kumuaga mtu yoyote, tena inaelezwa akiwa amepewa fdha ya kukata tiketike ya ndege kwenda kwao Zambia na kiongozi mmoja wa zamani wa Simba.
“Kweli Sunzu hayupo nchini, ameondoka zake na aliyempa fedha ya nauli tunamjua,” alisema mmoja we viongozi walio katika kamati za wa Simba.

“Unajua kuna kitu kimoja, kuna watu wanataka Simba ionekane imefeli baada ya wao kuondoka. Kweli wanatuumiza sana.


“Sasa Sunzu ameondoka lakini tunasikia kuna hujuma inaendelea kufanywa ili wachezaji waendelee kutuumiza. Si kitu chake.”

Inaelezwa, Sunzu ambaye alikuwa mchezaji analipwa mshahara mkubwa kuliko mwingine yoyote nchini, ameondoka mkataba wake ukiwa umebakiza mwezi mmoja tu.
Sunzu alikuwa analipwa dola 3,500 kwa mwezi, hivyo kuwa mchezaji ghali zaidi kuliko wote kwa maana ya mshahara katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Maana yake, hatarejea tena Simba, ingawa ilielezwa kulikuwa na juhudi zinafanywa kuhakikisha anarejea nchini kumalizia mechi zilizobaki ambazo zinaweza kuikoa Simba hadi kushika nafasi ya pili.

Hii ni mara ya pili kwa Sunzu kuondoka nchini. Miezi miwili iliyopita alirejea kwao Zambia, baadaye akaja nchini na baba yake mzazi ambaye aliomba kuvunja mkataba kwa madai mwanaye ni mgonjwa.

Simba waliafiki wakitaka kama atauzwa, basi nao walipwe. Lakini siku chache baada ya kurejea Zambia, alirejea nchini na kujiunga tena na Simba na ikaelezwa alikosa timu ya kucheza ndiyo maana akaamua kurudi tena Msimbazi.
 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic