Baada ya
upasuaji mkubwa uliofanyika kwa mafanikio makubwa, beki wa Yanga, Mbogo
Ladislaus, atafanyiwa upasuaji mwingine.
Mbogo
alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Mwananyama kuondoa uvimbe katika shavu
lake.
Lakini
amepangiwa kufanyiwa upasuaji mwingine katika shavu lake kwa lengo la kuondoa
ngozi ambayo ilitokana na upasuaji we awali.
“Kweli
daktari wa timu (Yanga), ameniambia kuna upasuaji unatakiwa kufanyika. Lengo ni
kurekebisha mambo yaende vizuri na mimi sina tatizo,” alisema Mbogo, baba wa watoto wawili.
Kuhusiana na
hilo, daktari wa Yanga, Nassor Matuzya alisema upasuaji wa pili utasaidia kurudisha
muonekano mzuri kwa Mbogo.
“Awali tulifanya zoezi la kuondoa nyama
iliyokuwa imevimba, kulikuwa na mafanikio makubwa, sasa kidonda kinakaribia kupona
na baada ya hapo tutafanya upasuaji mwingine kurudisha ngozi yake.
“Lazima
ngozi ya eneo hilo itakuwa imetanuka kwa kuwa ilikuwa na kitu ndani, baada ya
upasuaji wa pili tunaamini mambo yatakaa vizuri,” alisema Matuzya.
Mbogo
alilazimika kumhamishia mkewe Jema jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupata
huduma nzuri. Awali mkewe alikuwa akiishi jijini Mwanza ambao ni mji aliozaliwa
na kukulia kisoka beki huyo wa zamani wa Toto African.
0 COMMENTS:
Post a Comment