Saleh Ally
na Michuzi mdogo kabla ya mechi..
|
Waandishi
wanaimiliki timu blog mbalimbali, wameanzisha timu yao ya soka na leo imeanza
vizuri kwa kushinda mechi mbili na kupoteza moja.
Katika michuano
iliyopigwa kwenye Bonanza la Media Day leo kwenye Viwanja vya Leaders,
waandishi hao ‘Mablogga’, walionyesha ujuzi katika mechi zote walizocheza.
Walianza kwa
kupata ushindi wa chee baada ya Star TV kuingia mitini, wakapoteza mechi ya
pili kwa kufungwa mabao 3-0 dhidi ya Radio Maria iliyojaza mamluki wa kutosha.
Saleh Ally
chini ya ulinzi, kazi imeanza..
|
Lakini
iliporudi uwanjani, ikawatoa jasho DSJ, timu iliyokuwa imejaza vijana lukuki
ambao walionekana kama wanachezaki Ligi Daraja la Kwanza Bara, lakini wakalala
kwa mikwaju ya penalti.
Kwa mujibu
wa wadau wa timu hiyo, kama Issamichuzi, majjidmjengwa, salehjembe,
michuzijunior, binzubeiry, fatherkidevu, balilemajuto, michuzijr,sufianimafoto
na wengine, wamechukua uamuzi wa kuendeleza mazoezi kama kawa.
Angalia baadhi
ya picha za action, MABLOGGA walivyokuwa kazini...
Father Kidevu na Michuzi mdogo.. |
Penalti ya Bin Zubeiry inagonga mwamba ... |
Michuzi mdogo kazini... |
0 COMMENTS:
Post a Comment