April 13, 2013



Mshambuliaji wa zamani wa Prisons ya Mbeya, Yona Ndabila ni kati ya washambuliaji waliomaliza msimu wa Ligi Kuu Nepal kwa kuonyesha makali ya upachikaji mabao.

Ndabila ambaye aliwahi kuichezea Taifa Stars ikiwa chini ya Marcio Maximo, alifanikiwa kupachina mabao 16 na kushika nafasi ya pili kwa ufungaji.


Nafasi ya kwanza ilikwenda kwa mshambuliaji wa Three Stars ambao ndiyo waliibuka mabingwa huku timu ya Ndabila, Saraswat Youth Club ikishika nafasi ya tisa na kukosa nafasi ya kucheza nane bora.

Akizungumza na Salehjembe, Ndabila amesema anatarajia kurejea nchini humo Juni kujiandaa na ligi ambayo itaanza Julai.

“Niko nyumbani Mbeya nimekuja kuwaona wazazi, mwezi wa sita nitarejea kazini maana ligi inaanza mwezi wa saba,” alisema Ndabila.

Ndabila ambaye alionyesha kukata tamaa soka ya Tanzania, amekuwa mmoja wa wachezaji maarufu wa ligi hiyo.

Klabu yake imekuwa ikikataa kumuachia kutokana na kumuona ni tegemeo katika upachikaji wa mabao.

Kiana, hivi karibuni Ndabila alimvuta kiungo wa zamani wa Prisons, Yanga na Mbeya City, Godfrey Bonny ‘Ndanje’ ambaye pia ameanza kuonyesha makali yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic