April 8, 2013



Mtanzania Mbwana Samatta ameendeleza mguu wa mabao baada ya kupiga moja wakati timu yake ya TP Mazembe ilipoinyoa Muchudi ya Botswana mjini Lubumbashi kwa mabao 6-0.

Maana yake Mazembe ifuzu kwa jumla ya mabao 7-0 baada ya kushinda ugenini mjini Gaborrone kwa bao 1-0 ambalo lilifungwa na Samatta.
Kwa ushindi huo sasa Mazembe itakutana na wababe wa Afrika Kusini, Orland Pirates ya Soweto.


Timu hiyo kutoka katika kitongoji hicho maarufu zaidi nchini Afrika Kusini, ndiyo inayoongoza kwa kuwa na mashabiki wengi zaidi nchini humo.
Katika mechi ya jana, nahodha Tresor Mputu alifunga mabao mawili hivyo kuifanya Mazembe iweke rekodi mpya.

Mazembe imeweka rekodi ya kuwa moja ya timu zilizofanya vizuri zaidi tokea Shirikisho la Soka Afrika (Caf) lianze kutumia mfumo wa Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 1997 badala ya ule wa Klabu Bingwa Afrika uliokuwa ukitumika.

Tokea mwaka 1997 ilipoanza Ligi ya Mabingwa Afrika, Mazembe imeingia mara nane katika hatua ya 16 bora kama ilivyofanya safari baada ya kuinyoa Mochudi.

Wachezaji wa Mazembe ambao wamecheza michuano hiyo mara nyingi zaidi ni ni Mputu, Patou Kabangu na mshambuliaji Mzambia, Given Singuluma.

MATOKEO MENGINE YA LIGI YA MABINGWA...

 EST
1-0
Primeiro de Agosto 
 Orlando Pirates
2-1
Zanaco 
 Entente Setif
4 - 2
ASFA Yennega 
 Al Merreikh
1-2
Recreativo de Libolo 
 Al Hilal
3 - 1
Sewe San Pedro 
 Stade Malien
2-0
Casa Sport 
 AC Leopards
Vs
Kano Pillars 
 AS Vita Club
0 - 0
Zamalek 
 Rangers
2-0
Vital'O 
 Coton Sport
2-1 
AF Amadou Diallo  
 Asante Kotoko
1-1 
JSM Bejaïa 
 Union Douala
1-0 
FUS 
 Djoliba AC
1-1 
Saint George 
 Dynamos
1-0 
C.A.B 
 Al Ahly
2-0 
Tusker  
 TP Mazembe
6-0 
Mochudi C.Chiefs 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic