May 16, 2013



 
Kiungo nyota Mwingereza, David Beckham ametangaza kustaafu soka la ushindani.

Beckham amewashitua wengi kutokana na uamuzi wake huo wa ghafla huku akiwaacha midomo wazi PSG ambao walikuwa wamemuongezea mkataba wa mwaka mmoja.


Mwingereza huyo mwenye miaka 38, ametangaza kustaafu na kusema amefikia ndoto ya kila alichokitaka na sasa ni wakati wa kupumzika.



Akiwa na timu ya taifa ya England aliyowahi kuwa nahodha, Bekcham aliichezea mechi 115 na kuwa mmoja wa wachezaji waliocheza mechi nyingi wakiwa na timu ya taifa.

Hivi karibuni alitoa msaada mkubwa kwa PSG iliyofanikiwa kutwaa ubingwa wa Ufaransa baada ya kukaa ‘kapa’ bila kitu kwa miaka 19 iliyopita.

Beckham ndiye Mwingereza anayeshikilia rekodi ya kutwaa makombe manne katika nchi tofauti baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England akiwa na Man United, Real Madrid (Hispania), LA Galaxy na PSG (Ufaransa).

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic