May 16, 2013



 
Barcelona imepiga hatua katika uamuzi wake wa kutaka kumsaini mshambuliaji nyota kutoka Santos ya Brazil, Neymar.

Catalan tayari wamemuagiza mkurugenzi wa soka wa timu yao, Raúl Sanllehí ambaye hadi sasa yuko nchini Brazil kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu zaidi.


Pamoja na wapizania wao Real Madrid kuonyesha wanamtaka mchezaji huyo, lakini Barcelona walishatanguliza euro milioni 10 mwaka 2011.

Wakati Rais wa Barcelona, milione Sandro Rosell alikutana na makamu wa Rais wa Santos, Odilio Rodrigues Ijumaa iliyopita, lakini katika mkutano huo Raúl Sanllehí alihudhuria pia.

Siku chache baadaye Rosell alilaumiwa kwa kutotokea katika mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya katika mchezo wa kikapu kati ya Real Madrid na Barcelona, lakini baadaye ikagundulika alikuwa katika mkutano huo muhimu wa kuhakikisha anamnasa Neymar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic