Chelsea
ikiwa nyumbani imelazimishwa sare ya mabao 2-2 na wageni wake Tottenham
Hotspurs
Mchezo huo
ulioonekana ungetoa dira ya nani atashika nafasi ya tatu, umezidisha ugumu kwa
kuwa Chelsea wamefikisha pointi 69 wakiwa nafasi ya tatu, wanafuatiwa na
Arsenal wenye 67 na Spurs nafasi ya tano wakiwa na 67.
Mechi ilikuwa
ngumu nay a kuvutia huku mshambuliaji wa Spurs, Emmanuel Adebayor raia wa Togo
aking’ara kwa kufunga bao moja kutoa pasi ya bao la pili.
Tayari bingwa
ameishajulikana, lakini mshindi wa pili ni Man City, hivyo kuifanya nafasi ya
tatu kuwa ngumu zaidi na inayogombewa na timu tatu ambazo ni Chelsea, Spurs na
Arsenal.
MABAO YA CHELSEA:
Oscar 11,
Ramires 39.
MABAO YA SPURS:
Adebayor
26, Sigurdsson 80.
0 COMMENTS:
Post a Comment