Wakati Manchester United wakiwa wametangaza kwa asilimia 95 kuwa kocha wao mpya ni David Moyes, rekodi yake ya ugenini imeonekana kuzua mjadala.
Katika mechi
45 alizoiongoza everton dhidi ya timu kubwa za Man United, Chelsea, Liverpool
na Arsenal, hakuwahi kushinda hata mechi moja ya ugenini.
Katika mechi
hizo, Moyes alishindwa mechi 27 na sare 18 huku akiwa amepoteza 27 hivyo
kuanzisha hofu kwamba kama ataweza kuingoza United kushinda mechi zake za
ugenini.
Kwa kiasi
kikubwa kunaonekana kuwa na hofu kuhusiana na mambo yanavyokwenda na kama kocha
huyo atauweza muziki wa Man United.
Hofu nyingine
ni kuhusiana na michuano ya kimataifa barani Ulaya na inaonekana hana uzoefu,
kitu ambacho kitafanya alazimike kujifunza akiwa kazini.
REKOSI YA DAVID MOYES AKIWA EVERTON
P W D L Win%Everton 516 217 139 160 42.05
Rekodi ya ugenini dhidi ya Manchester United, Chelsea, Liverpool na Arsenal:
Cheza 45, Shinda 0, Sare 18, Poteza 27,
Pointi 18 (kati ya 135).
Pointi 18 (kati ya 135).
0 COMMENTS:
Post a Comment