May 16, 2013



 
Kuonyesha kwamba mechi ya keshokutwa haichukuliwi kiutani, kundi la Friends of Simba limeingia mzigoni baada ya kutua mjini Zanzibar.

Friends of Simba wametua mjini Zanzibar mchana huu wakiongozwa na
Mwenyekiti, Zacharia Hans Pope tayari kufanya mikakati zaidi ya ushindi dhidi ya Yanga keshokutwa Jumamosi.

Mmoja wa marafiki hao wa Simba amesema: “Tumefika Zanzibar, baada ya kufika tumepishana na timu inakwenda mazozini.


“Lakini jioni tutazungumza na vijana kwa ajili ya kupata dira, kwa kifupi tunataka kushinda mechi.”

Friends of Simba na uongozi wa Simba walikutana jana usiku baada ya mkutano wa kwanza kukwama baada ya Mwenyekiti Ismail Aden Rage kushindwa kutokea.

Timu hizo zinakutana katika mechi hiyo ya kufunga dimba la Ligi Kuu kila moja ikiwa na malengo yake.
Yanga ambayo tayari ni bingwa inataka kulipa kisasi cha mabao 5-0 huku Simba ikitaka heshima tu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic