May 14, 2013





Mchezo wa soka unapendwa kweli kuliko yote duniani, vijana wako tayari hata kuyatoa maisha yao ili waone mechi za soka.


Hii ilikuwa mwezi mmoja uliopita wakati Yanga ilipokwenda mjini Morogoro kuivaa Polisi ya mkoani humo kwenye Uwanja wa Jamhuri.

Kijana unayemuona hakujali hata kama anahatarisha maisha yake na badala yake akatembea kama ninja ukutani hadi alipofanikiwa kuingia ndani.


Hii ni zaidi ya kuruka ukuta na inataka mazoezi ya kutosha, lakini ameonyesha uwezo mkubwa maana hata wanaoigiza muvi kule Hollywood wanahitaji vifaa mahsusi ili wacheze michezo kama aliocheza yeye. Labda Jack Chain peke yake ndiye anaweza, duh!

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic