May 14, 2013



 
Nkongo aliyetolewa hatua ya mwisho akimuondoa kocha wa Simba...
Wakati joto la mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya mechi ya Simba na Yanga likizidi kupanda, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza waamuzi wa mchezo huo.


Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro ambapo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro. Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.


Hata hivyo, awali mwamuzi alikuwa Israel Nkongo lakini TFF imechukua uamuzi wa kumbadili baada ya gazeti la Championi kuandika mapema na kumhusisha na kumlima kadi nyekundu kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima katika mechi dhidi ya Azam FC iliyozya tafrani kubwa msimu uliopita.


Taarifa nyingine zinasema mwamuzi huyo amebadilishwa kutokana na kuwa na taarifa za ‘mchezo mchafu’ ambazo yeye alizishitukia na kukataa kupokea fedha kwa ajili ya kuibeba timu moja.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic