May 12, 2013



 Hatimaye mashabiki wa Manchester United wamepata bahati ya kumuaga kocha mkongwe nchini humo, Alex Ferguson ambaye ameitumikia klabu hiyo kwa miaka 27.

Dakika chache kabla ya mechi kati ya Man United dhidi ya Swansea kwenye Uwanja wa Old Trafford, Ferguson aliingia uwanjani na kuwaaga mashabiki hao ambao walikuwa wakimpungia mkono na kumshangilia kwa nguvu.

Baada ya hapo aliwasalimia mashabiki na kuweka saini yake katika vitabu, jezi, mipira kabla ya kwenda kukaa katika mechi na kuanza kushuhudia mechi hiyo dhidi ya Swansea.


Kocha David Moyes ndiye atachukua nafasi hiyo ya Ferguson na sasa yuko katika Uwanja wa Goodison Park ambako Everton inapambana na West Ham.



Moyes naye kabla ya kuanza mchezo huo, aliwaaga mashabiki wa Everton ambao amefanya nao kazi kwa miaka zaidi ya sita.
 
 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic