Kocha Mkuu wa TP Mazembe, Lamine Ndiaye ameamua kubwaga manyanga ikiwa ni siku chache baada ya timu yake kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mtanzania,
Mbwana Samatta ni kati ya washambuliaji tegemeo katika kikosi cha TP Mazembe,
pia Thomas Ulimwengu na wote wako katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars.
TP Mazembe
ilitolewa baada ya kushinda mechi yake ya pili kwa bao 1-0 wakati ilitakiwa
kushinda 2-0 dhidi ya Orlando Pirates ya
Afrika Kusini kwa mabao 3-1 jijini Johannesburg.
Ndiaye raia
wa Senegal ameamua kutangaza kujiuzulu kuifundisha timu hiyo baada ya kutolewa
kwa michuano hiyo na sasa imepangwa kushiriki Kombe la Shirikisho dhidi ya timu
ya Msumbiji.
0 COMMENTS:
Post a Comment